Jioni ya jana Wabunge Pamoja na Viongozi na wafanyakazi wa Taasisi ya Fountain Gate walijumuika katika makao makuu ya Bunge ili kushiriki katika kufuturu.
Kikao hicho kilicho andaliwa na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Fountain Gate Bwana Japhet Makau kiliwapa fursa wafanyakazi wa Bunge na wale wa Fountain Gate Academy kutangamana na viongozi wao.
Mgeni mwalikwa ambaye ni Spika wa bunge hakuweza kufika kutokana na sababu zisizo epukika ila aliweza kumtuma mwakilishi wake ambaye alimiminia sifa Taasisi ya Fountain Gate kwa ukarimu walionao na kuwahimiza viongozi wengine wauige mfano wa bwana Japhet Makau.